Rais Ndayishimiye Atembelea Ahadi: Vyama Visivyo na Viti Bungeni Vapatiwa Nafasi Kuu Serikalini

Raisi wa Burundi afanya uteuzi mipya

Katika hatua ya kihistoria ya kujenga mshikamano wa kitaifa, Rais wa Burundi Évariste Ndayishimiye ametekeleza ahadi yake ya baada ya uchaguzi kwa kuwateua wawakilishi kutoka vyama vitano visivyo na uwakilishi bungeni kushika nafasi za juu katika utawala wa mikoa. Uteuzi huu umetangazwa rasmi kupitia amri ya rais, na unahusisha mikoa mitano mipya iliyoundwa kufuatia mageuzi ya kiutawala ya mwaka 2025.


Nafasi Zilizotolewa: Mshauri wa Masuala ya Kijamii na Kitamaduni

Wateule hawa watashika nafasi ya Conseiller chargé des Affaires Sociales et Culturelles, nafasi yenye jukumu la kuratibu:


Mkoa Mteule Chama/Asasi
Bujumbura Micheline Bigirimana Florina
Buhumuza Oswald Ntakirutimana Sahwanya-FRODEBU
Butanyerera Manitwa Ndayubah UPD-Zigamibanga
Burunga Virginie Ndikumana APDR
Gitega Alice Nshimirimana MAC Société Civile

Ishara ya Ushirikishwaji wa Kisiasa

Kwa mujibu wa duru za serikali, uteuzi huu unaonesha dhamira ya kweli ya Rais Ndayishimiye ya kujenga taifa linalojumuisha wadau wote wa kisiasa, bila kujali uwakilishi wao bungeni. Hatua hii inakuja miezi michache baada ya uchaguzi mkuu wa Juni 2025, ambapo chama tawala CNDD-FDD kilishinda kwa zaidi ya 96% ya kura.


Maoni ya Wachambuzi

Wachambuzi wa siasa za Burundi wamekaribisha hatua hii kama ishara ya maridhiano ya kitaifa, ingawa wengine wanaona ni njia ya kisiasa ya kudhibiti upinzani kwa kuwapa nafasi zisizo na nguvu ya kisheria. Hata hivyo, uteuzi wa wawakilishi kutoka vyama tofauti unaonesha mwelekeo mpya wa kujenga utawala jumuishi.

picha-ndogo-ya-mwandishi by Twaha Ahmadi | Iliandikwa 27/07/2025

← Rudi Mwanzo Toa Maoni

Shiriki habari hii: